Breaking News

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO NOVEMBA 05, 2018


Sanamu mpya ya mshambuliaji Liverpool Mohamed Salah, 26, imewekwa nyumbani kwao huko Misri. (Liverpool Echo)

Mshambuliaji wa zamani wa LA Galaxy raia wa Sweden Zlatan Ibrahimovic, 37, huenda yuko njiani kurudi AC Milan kwa mkataba wa miezi sita. (Tuttosport, via Mirror)

Barcelona wameanza mazungumzo na waakilishi wa wing'a wa Chelsea raia wa Brazil William baada ya Chelsea kukataa ofa tatu msimu uliopita. (La Sexta, via Metro)

Beki wa Arsenal na Ufaransa Laurent Koscielny, 33, anawindwa na Barcelona, pamoja na mlinzi wa Chelsea raia wa Brazil David Luiz, 31. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Chelsea wako mbioni dhidi ya muda ikiwa wangetaka kumsaini kiungo wa kati Mreno Joao Felix, 18, baada ya Benfica kumpa mkataba mpya wenye kipenge cha kuondoka kwake cha kuvunja mkataba cha pauni 105. (Mirror)

Thorgan Hazard, ndugu wa kiungo wa kati wa Chelsea na Ubelgiji Eden Hazard anasema mchezaji huyo wa miaka 27 hawezi kuondoka Stamford Bridge kwenda Real Madrid mwezi Januari. (HLN, via Express)

Arsenal, Chelsea, Liverpool, ­Manchester City na Manchester United huenda wakachukuliwa hatua za kisheria kutoka kwa vilabu vilivyosalia vya Ligi ya Premier ikiwa watajiunga na Ligi iliyopendekezwa ya European superleague mwaka 2021. (iNews)

Wing'a wa Liverpool na Senegal Sadio Mane, 26, ametupilia mbali madai kuhusu hali ya mkataba wake, akisisitiza kuwa yuko na furaha huko Anfield. (Liverpool Echo)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anafikiria kumuacha nje Wing'a raia wa Uswizi Xherdan Shaqiri, 27, wakati wa mechi kati ya Liverpool na Red Star Belgrade wiki hii. Shaqiri amekuwa akikemewa na mashabiki wa Serbia kutokana na asilia yake ya Kosovo. (Telegraph)

Mlinzi wa zamani wa Manchester United Rio Ferdinand anasema mshambuliajia wa sasa wa Macnhester United Rashfold, 21, anahitaji kuwa katika kikosi cha kwanza cha mechi ikiwa angetaka kutumia uwezo wake huko Old Trafford. (BT Sport, via Manchester Evening News)

Mshambuliaji wa Juventus na Ureno Cristiano Ronaldo, 33, anasema amekosa sana kucheza na aliyekuwa mchezaji mwenzake huko Manchester United Wayne Rooney, 33, ambaye kwa sasa anaichezea DC United. (Express)

Meneja wa Napoli Carlo Ancelotti anaamini wachezaji wa PSG Neymar, 26, na Kylian Mbappe, 19, wanaweza kuwa warithi wa Cristiano Ronaldo na Lionel Messi. (Express)

Wolves, Crystal Palace na Southampton wote wanammezea mate mshambuliaji wa Leeds Kemar Roofe, 25. (Mirror, via Birmingham Mail) 

Meneja wa zamani wa Crystal Palace na Everton Sam Allardyce anasena wajukuu wake walidhulumiwa wakati akifutwa kama meneja wa England mwaka 2016. (Talksport)

Bora zaidi kutoka Jumapili
Mipango ya Manchester United kuwapa mikataba mipya kipa David de Gea, 27, na mshambuliaji Anthony Martial, 22, inatatizwa na mshahara wa pauni 400,000 aliopewa mshambuliaji Alexis Sanchez mwezi January. (Mirror)

Aaron Ramsey huenda akahamia Bayern Munich baada ya mabingwa hao wa Bendesliga kuonyesha nia ya kumsaini mchezaji huyo mweye miaka 27 wakati ataondoka Arsenal msimu ujao. (Express)
Meneja wa Chelsea Maurizio Sarri anasema viungo wa kati Danny Drinkwater, 28, na Victor Moses, 27, hawako kwenye mipango yake. (Evening Standard)

Chelsea na Manchester City wote wanataka kumsaini mchezaji wa Sunderland mwenye miaka 17, Bali Mumba ambaye amecheza mara nne tu kwenye klabu hiyo ya League One. (Sun)

Tottenham wanataka kumsaini kiungo wa kati wa Colombia Wilmar Barrios kutoka Boca Juniors mwezi Junuary. Mchezaji huyo mwenye miaka 25 anaweza kupatikana kwa puani milioni 16. (Star)
Serikali ya Uingereza itapinga mipango yoyote ya kubuniwa kwa Ligi nyingine ya Ulaya. (Telegraph)

No comments